Saturday, August 24, 2013

MAREKANI KUICHUKULIA HATUA SYRIA

Rais wa Marekani Barrack Obama amekutana na washauri wake wakuu wa masuala ya kiusalama kujadili madai ya matumzi ya silaha za kemikali nchini Syria.Maafisa wa Ikulu ya rais wamesema wanaangalia hatua kadhaa ambazo wanaweza kuchukua kuambatana na maslahi ya kitaifa ya Marekani na kutathmini vipi malengo yanaweza kuendelezwa nchini Syria. Duru zimearifu kuwa jeshi la Marekani limeanza kujiandaa kwa uwezekano wa kuishambulia Syria iwapo rais wao atatoa agizo hilo.Huku hayo yakijiri maafisa wakuu wa kijeshi kutoka Marekani,Uingereza na nchi kadhaa za Kiarabu wanatarajiwa kukutana mjini Amman Jordan kuzungumzia hali hiyo ya Syria ambapo mamia ya watu waliuawa kwa kile kinachoshukiwa kuwa matumizi ya silaha za kemikali karibu na mji mkuu Damascus.Utawala wa Syria leo umewashutumu waasi kwa mauaji hayo madai ambayo pia waasi inainyooshea kidole cha lawama serikali.Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa Angela Kane amewasili leo nchini Syria ili kuzungumzia uchunguzi wa matumizi ya silaha hizo.Rais wa Iran Hassan Rouhani amesema kuna ushahidi kuwa silaha hizo zilitumika na kulaani vifo vya raia.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO