Saturday, August 24, 2013

WANANCHI WA CONGO WAANDAMANA

Mamia ya raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameandamana kupinga mashambulizi yanayowalenga wakati wa makabiliano kati ya wanajeshi wa kikosi maalumu cha Umoja wa Mataifa na wapiganaji wa kundi la waasi la M23 katika mji wa Goma ulioko mashariki mwa nchi hiyo.Mwanamke mmoja na watoto wawili waliuawa mapema leo asubuhi katika mji huo wa Goma ambao ndio mji mkuu wa jimbo la Kivu ya Kaskazini.Wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wamekuwa wakijibu mashambulizi ya waasi wa M23 tangu Jumatano.Msemaji wa kikosi hicho maalumu Luteni Colonel Felix Prosper Basse amesema hali katika eneo hilo ni tete mno na kwamba shambulio hilo la hivi karibuni kabisa halikubaliki kamwe kwani linawalenga raia. Mapigano hayo yamewalazimu kiasi ya watu laki nane kutoroka makwao.Umoja wa Mataifa umetuma kikosi maalum cha wanajeshi 3,000 mashariki mwa Congo hususan kukabiliana na makundi ya waasi.Basse amesema wanashirikiana na wanajeshi wa nchi hiyo kuhakikisha usalama wa raia unadumishwa na kuahidi shambulio kama hilo halitafanyika tena. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO