Sunday, August 25, 2013

MAREKANI YALAANI SHAMBULIZI LA LEBANON

Serikali ya Marekani imelaani shambulizi lililotokea huko Lebanon na kusababisha vifo vya watu 42 mpaka sasa huku mamia wakijeruhiwa baada ya magari yalokuwa yameegeshwa nje ya msikiti kulipuliwa mjini Tripoli. Mshauri wa masuala ya usalama wa Marekani Susan Rice ameandika kupitia mtandao wa Twita kuwa Marekani imelaani vikali shambulizi hilo na kutoa pole kwa majeruhi na ndugu za watu wasiokuwa na hatia ambao walipoteza maisha yao. Mashambulizi hayo mawili yamejiri wakati wa ibada za waislamu mjini Tripoli ambapo wafuasi wa Suni ambao wanaunga mkono waasi wa Syria wamekuwa wakihusishwa na ghasia za mara kwa mara dhidi ya wale wanaomuunga mkono raisi wa Syria Bashar al Assad.
Serikali ya Washington mara kadhaa imevunja ukimya juu ya machafuko ya Syria na kuenea katika maeneo kadhaa na hususan kuvuruga amani ya lebanon. Naibu Msemaji wa serikali Marie Harf ametoa wito kwa pande zote mbili nchini Lebanon kuwa watulivu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO