Sunday, August 25, 2013

RAIS WA YEMEN AUNGA MKONO DRONE KUTUMIKA NCHINI HUMO

Rais Abd Rabbuh Mansur Hadi wa Yemen ameunga mkono mashambulizi ya mauaji ya ndege za Marekani zisizo na rubani yaani "drone" nchini humo. Mansur Hadi ameeleza kuwa mashambulizi ya drone za Marekani yanatekelezwa  kulingana na makubaliano yaliyosainiwa kati ya Washington na Ali Abdullah Saleh dikteta wa zamani wa Yemen baada ya mashambulizi ya Septemba 11 mwaka 2001.
Rais wa Yemen amesema hatua ya nchi yake ya kushirikiana na Marekani katika mapambano ya kile alichokitaja kuwa  dhidi ya ugaidi siyo siri. Ameongeza kuwa Yemen ina maafisa wake wa kijeshi katika vituo vya kuendeshea mashambulizi hayo ya drone nchini Djibouti na Bahrain. Marekani imekuwa ikikosolewa vikali kutokana na hatua yake ya kuzidisha mashambulizi ya ndege zisizo na rubani huko Yemen, ambako raia wa nchi hiyo wamekuwa wakiandamana mara kwa mara wakilaani hatua ya Washington ya kukiuka mamlaka ya kujitawala ya Yemen.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO