Sunday, August 25, 2013

PENTAGON YASEMA IKO TAYARI KWA LOLOTE JUU YA SYRIA

Chuck Hagel Waziri wa Ulinzi wa Marekani amekariri kwamba Pentagon imejitayarisha kuchukua chaguo lolote la dharura dhidi ya Syria na ipo tayari kutumia nguvu iwapo Rais Barack Obama ataidhinisha suala hilo.Hagel amesema kwamba, Rais Obama ameitaka Wizara ya Ulinzi ya Marekani kujitayarisha kwa chaguo lolote lile litakalowezekana kuchukuliwa dhidi ya Syria.
Waziri wa Ulinzi wa Marekani ameongeza kuwa, maafisa wa Marekani wanachunguza suala la kufanya mashambulizi ya kijeshi dhidi ya serikali ya Rais Bashar al Assad kutokana na ripoti ya kufanyika mashambulizi ya silaha za kemikali katika vitongoji vya Damascus wiki iliyopita.Hata hivyo ripoti zinasema kwamba, mashambulizi hayo ya silaha za kemikali yamefanywa na waasi wa Syria wanaoungwa mkono na nchi za Ulaya,  Marekani  na baadhi ya nchi za Kiarabu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO