Sunday, August 25, 2013

RAFAH YAFUNGULIWA TENA

Serikali ya mpito ya Misri leo imekifungua tena kivuko cha Rafah kilichoko kwenye mpaka wa pamoja wa nchi hiyo na eneo la Ukanda wa Gaza la ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Maelfu ya Wapalestina wakiwemo wanafunzi wa vyuo vikuu na wagonjwa wanaohitaji kupatiwa matibabu nje ya Ukanda wa Gaza walikuwa wameshindwa kuelekea huko Misri huku mamia ya Wapalestina waliokuweko nchini humo wakishindwa kurejea makwao kutokana na kufungwa njia hiyo pekee ya mpakani kwa wakaazi wa Gaza. Uhusiano kati ya serikali halali ya Palestina inayoongozwa na HAMAS yenye makao yake Ukanda wa Gaza na serikali ya mpito ya Misri umekuwa wa kusuasua tangu jeshi lilipomuondoa madarakani rais Muhammad Morsi aliyekuwa muitifaki mkubwa wa HAMAS. Maher Abu Sabha, afisa anayesimamia kivuko cha Rafah kwa upande wa Palestina amesema mamlaka za Misri zinakifungua kivuko hicho kwa muda wa saa chache tu kwa siku. Maafisa wa HAMAS wameilalamikia hatua ya serikali ya Misri ya kupunguza kiwango cha watu wanaoruhusiwa kupita kwenye kivuko cha Rafah kutoka watu 1,200 hadi 300 kwa siku tangu Julai 3 wakati jeshi lilipomuondoa madarakani Morsi. Tangu mwaka 2007, utawala wa Kizayuni umeshadidisha mzingiro dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina wanaoishi katika Ukanda wa Gaza na kusababisha maafa na matatizo makubwa kwa wananchi hao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO