Sunday, August 25, 2013

WAISLAM NIGERIA WAANDAMANA KUTAKA MORSI KUREJESHWA

Maelfu ya Waislamu wameandamana kwa amani kaskazini mwa Nigeria leo kutaka kurejeshwa madarakani kwa Rais wa Misri Mohammed Mursi aliyepinduliwa na jeshi mwezi uliopita.Kiasi ya waandamanaji 4,000 waliokuwa wamebeba mabango waliimba nyimbo za kumsifu Mursi nje ya msikiti katika mji wa Kano.Waandalizi wa maandamano hayo wanasema takriban waandamanaji 5,000 walishiriki.Kiongozi wa maandamano hayo sheikh Abubakar Mujahid amewaambia wanahabari kuwa wanataka kuachiliwa huru kwa Mursi na wafungwa wengine wa kisiasa wanaozuiliwa na serikali ya muda ya Misri.Nigeria taifa lililo na idadi kubwa zaidi ya watu barani Afrika ya kiasi ya watu milioni 160 limegawanyika nusu kwa nusu ambapo Waislamu wanaishi hasa kaskazini  na Wakristo wanaokaa zaidi kusini mwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO