Tuesday, July 01, 2014

CHINA KUJENGA JENGO LA 1KM KWA UREFU

China ipo katika mkakati wa ujenzi wa jengo refu kuliko yote duniani litakaloitwa ''Phoenix tower''. Jengo hilo linatarajiwa kumalizika kati ya mwaka 2017/2018 kuanzia ujenzi wake. jengo hilo litakalojengwa katika jimbo la  Hubei katikati mwa china linatarajiwa kuwa la kuvutia lenye rangi ya pink na litakuwa rafiki wa mazingira. Inategemewa jengo hilo litazidi jengo refu liliopo sasa la Buruj Khalifa kwa mita 172.
''Kutakuwa na mtaa wa Kifaransa, mtaa wa Kijapani, na hata mtaa wa Kituruki na mitaa mingine mingi zaidi amdayo itaruhusu watu kuiona dunia bila ya kuondoka China'' alisema Chetwood kuiambia ''The Guardian''. Mpaka sasa kuna ujenzi wa majengo mengi marefu yanayoshindana duniani ikiwemo Buruj Khalifa liliopo Dubai, na jingine ambalo ujenzi wake unategemewa kukamilika mwaka 2019 nchini Saudi Arabia litakaloitwa ''Kingdom tower'' na hili la nchini China.

Chanzo: CNN

 Hili ndo jengo refu kwa sasa la Buruj Khalifa huko Dubai


Hili ni jengo litakalo jengwa nchini Saudi Arabia litakaloitwa Kingdom Tower.





No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO