Thursday, July 03, 2014

WANASAYANSI WAGUNDUA UCHAPISHAJI WA MISHIPA YA DAMU

Ogezeko la maendeleo ya kiteknolojia yamepelekea watu kufikiri njia mbadala za kurahisisha maisha zaidi. Katika swala la afya, tunashuhudia ugunduzi mkubwa wa kitabubu ambapo wanasayansi kutoka maeneo mbalimbali duniani wantumia muda wao mwingi katika utafiti. Mpaka leo bado kuna uhaba wa viungo vya binaadamu ambapo watu wengi wamekuwa wakipoteza maisha kutokana na uhaba huu. Njia inayotumika mpaka sasa ni ya kupewa viungo mfano wa figo kutoka kwa mtu mwingine. Miaka ya karibuni, watu walizindua mashine za uchapishaji wa vitu halisi yaani "3D printing". Sasa teknolojia hiyo inaunganishwa na afya kwa ajili ya kuchapisha viungo vya mwili "BioPrinter". Inashangaza lakini ni wazo zuri, fikiria mfano unaenda hospitali na unahitajika ufanyiwe upasuaji wa figo, bila kusita wala kutafuta mtu wa kukupa figo yake, basi inaenda kuchukuliwa kutoka kwenye maabara tu. Kwa sasa watafiti kutoka vyuo vya Sydney, Harvard, Stanford na MIT wamefanikiwa kugundua uchapishaji wa mishipa ya damu hasa katika mapafu. Wametumia utafiti wao na njia mbali mbali za kitabibu hatimae wamefanikiwa kuchapisha mfumo wa mishipa midogo sana ya damu ndani ya mapafu. 

Chanzo: Engadget

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO