Friday, July 11, 2014

MASHAMBULIZI YA WAISRAEL KATIKA MSIKITI WA AL-AQSA


Wakati waislamu wote duniani waiwa katika mfungo wa Ramadhani, Wapalestina na maeneo mengine yenye waislamu hayana furaha. Tunashuhudia kwa siku ya pili sasa mauaji ya wanawake na watoto yakiedelea huko Gaza nchini Palestina. Hii ni moja ya video zilizosambaa mitandaoni ikionesha mashambulizi katika msikiti wa Al-Aqsa, miongoni mwa maeneo matukufu kwa waislamu. Jeshi la Israel ndo linatekeleza mashambulizi hayo bila huruma wala aibu yoyote ile huku taasisi za umoja wa mataifa na tasisi za haki za binaadamu zikikaa kimya kabisa. Pia vyombo vya habari tunavyovijua vya kimataifa vimekuwa washabiki wa upande mmoja wa habari, vikionesha kama vile israel imekuwa ikionewa wakati huohuo havioneshi ni jinsi gani wapalestina wakiuwawa hasa wale wasiokuwa na hatia kabisa kwani mashambulizi yamekuwa yanafanyika katika makazi ya watu na sio katika maeneo ya kivita. Mungu Awafanyie wepesi watu wa Palestina na audhalilishe utawala haramu wa kizayuni. Ameen!!  

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO