Friday, November 30, 2012

BARAZA LA WAASISI MISRI LAPASISHA RASIMU YA KATIBA


Baraza la Waasisi la Misri limepasisha vipengee vya rasimu ya katiba mpya ya nchi hiyo katika kikao kilichofanyika jana.
Moja ya vipengee muhimu vya rasimu ya katiba mpya ya Misri ni kile kinachosisitiza kuwa sheria za Kiislamu ndio marejeo ya sheria zote za nchi hiyo. 


Rasimu ya katiba mpya ya Misri pia inasisitiza kuwa kipindi cha urais wa nchi sasa kitabanwa katika duru mbili, tofauti na ilivyokuwa katika utawala wa dikteta wa zamani wa nchi hiyo ambaye aliiongoza Misri kwa zaidi ya miaka 30. Rasimu hiyo itawasilishwa kwa Rais Muhammad Mursi ambaye baada ya kuipasisha ataitisha kura ya maoni ya wananchi na kuwa katiba mpya ya nchi hiyo.
Katiba ya zamani ya Misri ilibatilika baada ya mapinduzi ya wananchi ya mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO