Friday, November 30, 2012

KATIKA KUMBUKUMBU YA LEO IJUMAA


Leo ni Ijumaa tarehe 16 Muharram 1434 Hijria, sawa na tarehe 30 Novemba 2012 Miladia.



Siku kama ya leo miaka 24 iliyopita aliaga dunia ustadh na karii mashuhuri wa Qur'ani Abdul Basit Muhammad Abdul Samad katika mji mkuu wa Misri, Cairo. Alianza kujifunza Qur'ani Tukufu akiwa bado mtoto mdogo na alipewa tuzo ya kuhifadhi na kusoma Qur'ani akiwa na umri wa miaka 12. Kipindi fulani Ustadh Abdul Basit alitumia muda wake mwingi kusafiri katika nchi za Kiislamu na kuwahamasisha watu kusoma kitabu cha Mwenyezi Mungu. Ustadh Abdul Basit ameacha kanda nyingi za Sauti ya kiraa yake ya Qur'ani Tukufu ambazo bado zinawavutia wasomaji wengi wa Qur'ani.


No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO