Tuesday, November 27, 2012

NYEPESI KUTOKA TUME YA KATIBA LEO ASUBUHI


Pamoja na maoni hayo, kuna matukio mawili yaliyojitokeza leo yanafaa ku-share na wengine.


LA KWANZA: Hili limetokea asubuhi Welezo ambapo Mzee Warioba alikuja kujumuika na wana-Tume iliyopo Zanzibar. Mwana-Mkataba mmoja alihoji vipi Wazanzibari waendelee na mfumo uliopo wakati nafasi zote kubwa kubwa katika mihimili mbali mbali ya Dola zinashikwa na watu wa Tanganyika tu.

 Mzee Warioba kama kawaida yake huwa hawezi kustahamili mawazo yasiyokubaliana na yake, akamwambia hivi hajui Tume ya Katiba Makamu Mwenyekiti wake ni Mzanzibari? Mwana-Mkataba akamjibu hivi huyo Jaji Agostino Ramadhani hana sifa za kuwa Mwenyekiti na wewe ukawa chini yake? Mzee Warioba akagwaya. Kimya!


LA PILI: Hili limetokea jioni Welezo. Mwana-Mkataba mmoja alipozungumzia Zanzibar kuwa na mamlaka kamili na Rais wa Zanzibar awe na hadhi kamili kama Mkuu wa Nchi ndani na nje. Mwenyekiti wa Timu iliyopo Zanzibar, Prof. Mwesiga Baregu akamwambia hivi sasa Rais Shein yupo Vietnam, kenda kama Rais.

 Mwana-Mkataba akamjibu kenda kama Rais lakini baada ya kupata kibali cha Waziri Benard Membe na kumuuliza na Rais wa nchi gani anayehitaji kibali cha Waziri ili apokelewe kama Rais? Prof. Baregu akabaki kimya!

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO