Wednesday, November 28, 2012

SUSAN RICE AKIRI ALIONGOPA KUHUSU KUUAWA BALOZI WA MAREKANI LIBYA

Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Susan Rice amekiri kwamba alitoa taarifa ya uongo kuhusu matukio yaliyopelekea kuuawa balozi wa nchi yake huko Libya miezi kadhaa iliyopita. Awali Rice alikuwa amesema shambulio dhidi ya ubalozi mdogo wa Marekani mjini Benghazi, Libya lilikuwa la kigaidi lakini mwishoni mwa wiki alikiri kwamba, waandamanaji wa Kiislamu waliokuwa na hasira baada ya kuonyeshwa filamu inayomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW ndio waliovamia ubalozi huo na kuuchoma moto. Amesema Waislamu walikuwa na haki ya kuonyesha hasira zao lakini akadai kwamba walichupa mipaka katika kuelezea ghadhabu zao.

Matamshi ya Rice yamemuweka katika hali ngumu na Wabunge wa upinzani wameapa kukabiliana na juhudi zozote za Rais Barack Obama za kumteua kuwa Waziri wa Mambo ya Nje baadaye mwaka ujao. Rice alikuwa amepigiwa upatu kuchukua nafasi ya Hillary Clinton anayemaliza muda wake mapema mwaka ujao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO