Thursday, November 29, 2012

UN KUPIGA KURA YA PALESTINA

Rais wa Palestina Mahmud Abbas anapanga leo kushinikiza kupitishwa kura ya Umoja wa Mataifa ya kuitambua Palestina kama taifa. Ujerumani haitaunga mkono jitihada za Palestina za kutaka hadhi ya dola mwangalizi ndani ya Umoja wa Mataifa. Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lenye nchi wanachama 193 linatarajiwa kupiga kura kwa wingi kuunga mkono ombi hilo, ambalo litaipa Mamlaka ya Palestina kibali cha kujiunga na mahakama za kimataifa kama vile Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita mjini The Hague, Uholanzi. Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Hillary Clinton anasema msimamo wao haubadiliki. Kuna wasiwasi miongoni mwa wanaounga mkono Israel kwamba Wapalestina watajaribu kuishitaki nchi hiyo ya Kiyahudi kwa uhalifu wa kivita katika mahakama ya ICC. Ombi la Palestina limeugawanya Umoja wa Ulaya, huku Ujerumani na Uingereza zikisema zitasusia kura hiyo nayo Ufaransa ikisema itaunga mkono jitihada hizo za kutaka hadi ya uangalizi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO