Thursday, November 29, 2012

MASHAMBULIO YA KIGAIDI DHIDI YA WAISLAM MAREKANI


Polisi ya jimbo la Texas nchini Marekani inamshikilia raia mmoja wa nchi hiyo kwa tuhuma za kutaka kuwashambulia waumini wa Kiislamu waliokuwa wakisali Msikitini. Polisi ya Texas imeeleza kuwa, Christopher Bane mwenye umri wa miaka 44 anashikiliwa na jeshi la polisi katika jimbo hilo kwa kosa la kutaka kuwafyatulia risasi Waislamu waliokuwa ndani ya Msikiti mmoja katika mji wa San Antonio. Taarifa za polisi zinasema kuwa, Christopher Bane alikuwa na azma ya kuwashambulia Waislamu hao na kisha ajiuwe. Polisi ya Texas imeeleza kuwa, msamaria mwema mmoja alitoa taarifa hizo kituoni za kutaka kushambuliwa Waislamu. Kabla ya hapo, ofisi ya Baraza la Mahusiano ya Kiislamu nchini Marekani katika jimbo la Chicago lilitangaza kushambuliwa Msikiti mmoja ulioko katika mji wa Morton Grove. Baraza hilo limeongeza kuwa, katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita, Misikiti miwili iliteketezwa moto katika jimbo la Missouri nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO