Thursday, November 29, 2012

WAFUNGWA 3,800 WALIOHUKUMIWA KIFO WAPELEKWA SYRIA

Mkuu wa Shirika la Habari la Iraqi al Nakhil amesema kuwa nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi zimewatuma nchini Syria wafungwa 3,800 waliohukumiwa adhabu ya kifo kwa shabaha ya kupigana dhidi ya serikali ya Rais Bashar Assad wa nchi hiyo.




Muhammad Ali al Hakim amesema kwamba, hadi sasa wafungwa 3,800 waliohukumiwa adhabu ya kifo katika baadhi ya jela za nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi ikiwemo Qatar, Saudi Arabia na Kuwait wameachiliwa huru na kupelekwa  nchini Syria ili kutekeleza operesheni za kigaidi.
Mkuu wa shirika la habari la Iraq al Nakhil amesema, Walid Twabatwabai mwakilishi wa Masalafi katika Bunge la Kuwait ndiye anayegharamia kupelekwa wafungwa hao wa Kiarabu nchini Syria kutekeleza operesheni za kigaidi. Walid Twabatwabai miezi mitatu iliyopita aliitembelea Syria na mbali na kushiriki katika maandamano dhidi ya serikali ya Rais Bashar al Assad wa nchi hiyo alitangaza kuwa yuko tayari kutoa fedha na kuunga mkono magaidi nchini humo.
Kwa miezi kadhaa sasa Syria inakabiliwa na machafuko ambapo makundi ya kigaidi yanayoungwa mkono na nchi za kigeni yanapigana dhidi ya serikali ya Damascus.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO