Thursday, December 27, 2012

JUMLA YA WATOTO 41 WALIUWAWA KWA MASHAMBULIO YA ISRAEL DHIDI YA HAMAS

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadmau Amnesty International limethibitisha kwamba watoto 41 wa Kipalestina waliuawa katika mashambulizi ya siku 8 yaliyofanywa na majeshi ya utawala wa Israel katika eneo la Ukanda wa Gaza. Taarifa iliyotolewa leo na shirika hilo imeeleza kuwa, maafa yaliyosababishwa na majeshi ya Israel katika kipindi cha siku 8 ni makubwa zaidi kuliko mashambulizi yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka 2008 huko Gaza. Amnesty International imeeleza kuwa, mauaji dhidi ya watoto katika vita vya utumiaji silaha, yanahesabiwa kuwa jinai kubwa dhidi ya binadamu. Amnesty International imezitaka kamati maalumu za Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na asasi nyingine za kimataifa kuendeleza uchunguzi wao kuhusiana na mashambulizi ya Israel dhidi ya raia wa Palestina wa eneo la Gaza. Serikali ya Palestina iliyochaguliwa na wananchi na inayoongozwa na Hamas imeeleza kuwa, mashambulizi ya siku 8 huko Gaza yalipelekea watu 185 kuuawa shahidi na wengine 1,399 kujeruhiwa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO