Thursday, December 27, 2012

MAREKANI KUTUMA MAJESHI NA MAJASUSI AFRIKA


Utawala wa Marekani umetangaza mpango wa kutuma majasusi barani Afrika baada ya kuidhinisha mpango mwingine wa kutuma wanajeshi 4,000 katika nchi 35 za bara hilo. Imearifiwa kuwa Wakala wa Kijasusi katika Jeshi la Marekani DIA imeshaanza kutuma majasusi wa kijeshi katika maeneo mbali mbali ya Afrika.
Hatua hiyo inaashiria kuwa Marekani ina njama kubwa zaidi kuliko inavyodai kuwa lengo lake ni kutoa mafunzo kwa wanajeshi katika nchi za Afrika. Marekani imeimarisha mikakati yake ya kijeshi barani Afrika baada ya kushuhudiwa mwamko mkubwa wa Kiislamu katika nchi za Afrika Kaskazini. Mwamko huo wa Kiislamu umepelekea kutimuliwa madarakani madikteta waliokuwa vibaraka wa Marekani huko Tunisia, Misri na Libya. Hivi karibuni serikali ya Marekani ilisema inakusudia kutuma majeshi yake katika nchi 35 za Kiafrika kwa kisingizo cha kukabiliana na tishio la vitendo vya kigaidi barani humo. Wanajeshi hao wa Marekani watatumwa katika nchi za Afrika Mashariki kama vile Kenya na Uganda.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO