Thursday, December 27, 2012

SOMALI YAWATAKA AL SHABAAB KUWEKA SILAHA CHINI


Somalia imewapa muda wa siku 120 wapiganaji wa as Shabab ili waweke silaha zao chini na kujiunga na mpango wa amani na kujenga taifa. Abdikarim Guled Waziri wa Mambo ya Ndani na Usalama wa Taifa wa Somalia amesema kuwa, serikali pia imewataka vijana wanaopigana katika kundi hilo wajisalimishe na kuondoka kwenye kundi hilo.
Aidha amewataka wapiganaji wa as Shabab kuacha fikra za kuzusha machafuko na vita, na kuahidi kuwa serikali itawasamehe vijana watakaojisalimisha, kwani wamelaghaiwa na kutiwa kasumba.
Taarifa zinasema kuwa, wafuasi wasiopungua 550 wa kundi la as Shabab hadi sasa wamelikimbia kundi hilo na kujisalimisha kwa maafisa wa serikali ya Somalia. Kundi hilo mwaka 2006 lilijitoa katika Muungano wa Mahakama za Kiislamu (UIC) na kuanza harakati na mapigano kwa lengo la kuangusha serikali ya mpito ya Somalia.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO