Saturday, December 29, 2012

M23 WASHAMBULIA HELIKOPTA YA UN

Kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kimesema kuwa waasi wa harakati ya Machi 23 wamezishambulia helikopta zake mbili huko mashariki mwa Kongo. Ujumbe wa Umoja wa Mataifa Monusco umesema katika taarifa yake ya jana kwamba helikopta mbili za umoja huo zilishambuliwa Jumatano usiku iliyopita katika anga ya miji ya Kibumba na Kanyamahahoro inayodhibitiwa na waasi wa M23.
Taarifa ya Monusco imeongeza kuwa hii ni mara ya pili kwa waasi wa Machi23 kuzishambulia helikopta za Umoja wa Mataifa kwa makusudi na kwamba wale waliohusika watachunguzwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria. Hata hivyo Luteni Kanali Vianney Kazarama msemaji wa waasi wa harakati ya M23 amekanusha madai kuhusu kushambuliwa helikopta hizo za Umoja wa Mataifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO