Wednesday, December 26, 2012

MAANDALIZI YA KUKUSANYA SILAHA YAANZA LIBYA

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Libya imetangaza kuwa inatayarsha mpango kwa ajili ya kukusanya silaha haramu na kusambaratisha makundi ya wanamgambo ili kurejesha amani na usalama nchini humo. Majdi al A'rafi msemaji wa wizara hiyo ametangaza kuwa, mpango huo unatayarishwa kwa ushirikiano na mkuu wa vikosi vyote vya jeshi la Libya na kwa uungaji mkono wa taasisi za kiraia, mashekhe, wafanyabiashara tofauti na vyombo vya habari vya nchi hiyo.
 Afisa huyo wa Libya ameongeza kuwa, kuwepo silaha mikononi mwa raia kinyume cha sheria kunakwamisha jitihada za serikali za kutekeleza mipango ya maendeleo, kwani mashirika ya kigeni yaliyokuwa yakijishughulisha na shughuli tofauti za kimaendeleo kabla ya mapinduzi ya Libya zenye thamani ya mabilioni ya dola hivi sasa hayako tayari kurejea nchini humo kutokana na ukosefu wa usalama.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO