Wednesday, December 26, 2012

WAMAREKANI WASHAMBULIWA TENA AFGHANISTAN

Bomu la kutegwa garini limelipuka karibu na kambi ya kijeshi ya Marekani mashariki mwa Afghanistan na kupelekea watu wasiopungua watatu kuuawa na wengine 7 kujeruhiwa. Sediq Sediqqi Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Afghanistan amesema kuwa, mlipuko huo umetokea katika lango la Kambi ya Chapman ya Marekani kwenye mji wa Khost nchini humo. Kundi la Taliban limetangaza kuhusika na shambulizi hilo ambapo msemaji wa kundi hilo Zabihullah Mujahid amesema, limefanywa ili kuwalenga wale wanaowahudumia Wamarekani katika kambi hiyo. Mlipuko huo umetokea siku moja baada ya polisi mmoja wa kike wa Kiafghani kumuua mshauri wa polisi ya Marekani katika makao makuu ya polisi mjini Kabul. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO