Friday, December 28, 2012

KAMANDA ALIYESAIDIA KUMUONDOA SADDAM HUSSEIN KUWAIT AFARIKI

Norman Schwarzkopf, Jenerali wa Marekani aliyeongoza Operesheni ya kijeshi iliyopewa jina la Uvamizi wa Jangwani, ambayo iliikomboa Kuwait kutoka mikononi mwa kiongozi wa Ki imla wa Iraq Saddam Hussein mnamo mwaka wa 1991, ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 78. Schwarzkopf, amefariki mjini Tampa, ambako alistaafu baada ya jukumu lake la mwisho kama Kamanda Mkuu wa Jeshi la Marekani. Rais wa zamani George H W Bush ambaye kwa sasa yuko katika chumba cha wagonjwa mahututi katika jimbo la Texas, amekuwa wa kwanza kutoa taarifa ya kuomboleza kifo cha mtu ambaye yeye alimchagua kuongoza vita ambavyo vilizipa sifa taaluma zao wote wawili. Taarifa hiyo ya Bush imemtaja Schwarzkopf kama mzalendo halisi wa Marekani na mmmoja wa viongozi wakuu wa kijeshi katika kizazi chake. Jeshi la Saddam Hussein lililokuwa na watu milioni moja liliivamia Kuwait mnamo mwaka wa 1990 na kuonekana kutaka kuingia Saudi Arabia, jambo ambalo lingempa zaidi ya asilimia 40 ya hifadhi za mafuta ulimwenguni. Schwarzkopf aliliweka pamoja jeshi la washirika kutoka nchi 32, ambalo liliviondoa vikosi vya Iraq nchini Kuwait katika wiki chache kupitia mashambulizi makali ya kutokea angani na nchi kavu

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO