Friday, December 28, 2012

MUBAARAK ALAZWA TENA HOSPITALI

Maafisa nchini Misri wamesema rais aliyeondolewa madarakani Hosni Mubarak amehamishwa kutoka gerezani ambako anatumikia kifungo cha maisha, na kupelekwa katika hospitali ya kijeshi kupokea matibabu. Mubarak amerudishwa hospitalini baada ya hali yake ya kiafya kuwa mbaya. Wiki iliyopita, rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 84 alipelekwa katika hospitali hiyo hiyo kufanyiwa vipimo vya matibabu kutokana na ma majeraha aliyopata ya kichwa na mbavu baada ya kuanguka. Mnamo mwezi Juni, Mubarak alilazwa hospitalini kwa mwezi mmoja baada ya kudaiwa kukosa fahamu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO