Friday, December 28, 2012

WAFANYAKAZI WAGOMA ISRAEL

Idadi kubwa ya wafanyakazi wa shirika la bima la utawala wa Kizayuni wa Israel wamefanya mgomo kulalamikia ugumu wa kazi, mazingira mabaya ya kazi na kutopandishwa mishahara yao. Redio ya kijeshi ya utawala huo imetangza kuwa, wafanyakazi hao wamefanya mgomo hii leo baada ya kushindikana kufikiwa makubalino kati yao na serikali ya utawala huo bandia. Hadi sasa viongozi wa Israel, wanafanya juhudi za kufanyika mazungumzo na viongozi wa shirika la bima kwa ajili ya kumaliza mgomo huo. Kabla ya hapo wafanyakazi hao walifanya mgomo kulalamikia kiwango duni cha mshahara walichosema hakilingani na kazi wanazozifanya, mgomo ambao pia ulijiri baada ya kushindikana kupatikana mwafaka kati yao na Wizara ya Fedha ya Utawala huo wa Kizayuni. Ni vyema kuashiria hapa kuwa, utawala katili wa Kizayuni hivi sasa unakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi ambayo imeufanya ushindwe kumaliza vilio vya wafanyakazi wake. Ni hivi karibuni tu utawala huo pia ulishuhudia mgomo wa wauguzi wapatao elfu 28 uliosababisha kusitishwa shughuli za operesheni za upasuaji katika hospitali zake zipatazo elfu 10.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO