Thursday, January 31, 2013

ARGENTINA YAKATAA OMBI LA ISRAEL KUHUSU IRAN


Argentina imekataa ombi la Israel la kutaka ipewe maelezo juu ya makubaliano yaliyofikiwa hivi karibuni kati ya nchi hiyo na Iran ya kuchunguza mlipuko wa mwaka 1994 huko Buenos Aires ulioua watu 85. Wizara ya Mambo ya Nje ya Argentina imesema, ombi hilo la Israel si sawa na linapingwa vikali. Taarifa ya wizara hiyo imesema, shambulio la kigaidi la Julai 18, 1994 halikumhusu hata raia mmoja wa Israel kwani wahanga wote walikuwa raia wa Argentina, Bolivia, Poland na Chile.
Jumapili iliyopita Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Ali Akbar Salehi na mwenzake wa Argentina walisaini makubaliano ya maelewano kati ya pande mbili kuhusiana na kuchunguzwa zaidi mashambulizi hayo ya kigaidi yaliyotokea huko Buenos Aires mwaka 1994. Huko nyuma na chini ya mashinikizo ya Marekani na Israel Argentina iliituhumu Iran kuhusika katika mashambulizi hayo, madai ambayo yalikanushwa vikali na Tehran.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO