Thursday, January 31, 2013

NIGERIA KUPOKEA NDEGE ZA KUJASUSI TOKA MAREKANI


Waziri wa Ulinzi wa Niger ametangaza kwamba, nchi yake ipo tayari kuanzisha kituo cha ndege zisizo na rubani za Marekani ili kuisaidia Washington kufanya ujasusi barani Afrika. Karidjo Mahamadou amesema, nchi hiyo pia itakubali msaada wa ndege kwa ajili ya kusimamia harakati zinazotia shaka nchini Mali. Hata hivyo amesema kuwa, hana taarifa juu ya makubaliano yoyote kati ya nchi yake na Marekani kwa ajili ya kupelekwa ndege kama hizo nchini Niger.
Iwapo mpango huo utatekelezwa, utadhihirisha hatua nyingine ya Marekani ya kutaka kujiimarisha kijeshi barani Afrika.
Marekani hivi karibuni ilitangaza mpango wa kupeleka vikosi maalumu vya jeshi katika nchi 35 za Kiafrika.  Marekani ina kituo cha kudumu cha kijeshi nchini Djibouti.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO