Saturday, January 26, 2013

MMAREKANI AHUKUMIWA MIAKA 494 JELA

Mahakama katika jimbo la Pennsylvania nchini Marekani imemuhukumu Walter Meyerle mwenye umri wa miaka 36 adhabu ya kifungo cha miaka 494 jela, baada ya kupatikana na kosa la kubaka na kuwadhalilisha kijinsia watoto 15 nchini humo. Mahakama hiyo imeeleza kuwa, kuanzia mwaka 1997 hadi 2010 Walter Meyerle aliwabaka watoto wavulana na wasichana wenye umri wa kati ya miaka  4 na 17. Mwendesha mashtaka wa kesi hiyo amesema kuwa, idadi kubwa ya watoto hao waliofanyiwa unyama huo walikuwa ni watoto wa marafiki zake. Wakati huohuo, Mahakama ya Chicago imempiga faini ya dola laki tano  mwalimu Kevin Jones baada ya kupatikana na hatia ya kuwadhalilisha wanafunzi wake. Mmoja kati ya mwanafunzi aliyekuwa mhanga wa kutumiwa vibaya kijinsia na mwalimu Kevin Jones alitoa ushadidi wake huo kwenye mahakama hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO