Friday, January 25, 2013

UN YARIDHIA DRONE KUTUMWA KONGO

Baraza la Umoja wa Mataifa limeidhinisha matumizi ya ndege zisizo na rubani, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, baada wiki kadhaa za ucheleweshwaji kufuatia wasi wasi wa Urusi, China na Rwanda juu ya matumizi ya ndege hizo za uchunguzi. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ban Ki-Moon aliliandikia Baraza hilo mwishoni mwa mwezi uliyopita, kushauri kuwa walinda amani nchini Kongo wanapanga kutumia ndege hizo kuboresha uwelewa wa hali ya huko na kuharakisha mchakato wa maamuzi katika kushughulikia uasi wa kundi la M23. Rais wa baraza hilo kwa mwezi huu wa Januari, balozi wa Pakistan katika Umoja wa Mataifa Masood Khan amemjibu Katibu Mkuu Ban kuwa wamepokea maombi hayo na kuyaridhia. Lakini baraza hilo limesema ndege hizuo zitatumika tu kwa majaribio.
 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO