Friday, January 25, 2013

MATAIFA YA MAGHARIBI YATAKA RAIA WAKE KUONDOKA BENGHAZI

Uingereza, Ujerumani, Uholanzi na Australi zimewataka raia wake kuondoka katika mji wa Benghazi mashariki mwa Libya, kutokana na kitisho dhidi ya raia wa nchi za Magharibi, kinachohusishwa na kuingilia kijeshi kwa Ufaransa katika mgogoro wa Mali. Onyo la Uingereza lililotolewa jana Alhamisi liliikasirisha serikali ya Libya, iliyosema kuwa hakukuwa na taarifa mpya za uchunguzi kuhalalisha wasi wasi huo mjini Benghazi. Idara ya mambo ya nje ya Australia imesema kuwa wanatambua tishio maalumu kwa raia wa nchi za Magharibi mjini Benghazi, na kuwataka raia wake kuondoka huko mara moja. Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron alionya wiki iliyopita kuwa kilichotoekea nchini Algeria katika kiwanda cha gesi ni sehemu tu ya vita virefu dhidi ya magaidi wauaji duniani kote. Jana Alhamisi, Ujerumani na Uholanzi pia ziliwaonya raia wake na kuwataka waondoke mara moja kutoka Benghazi. Lakini naibu waziri wa mambo ya kigeni wa Libya, Abdullah Massoud alielezwa kusikitisha kwake juu ya onyo hizo, na kusema kuwa serikali mjini Tripoli itahitaji maelezo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO