Friday, January 25, 2013

MISRI YAUPINGA MKATABA WA AMANI WA CAMP DAVID

Duru za kidiplomasia kutoka Cairo zinaeleza kuwa, serikali ya Misri imetupilia mbali takwa la Marekani la kuitaka serikali hiyo ifungamane kikamilifu na makubaliano ya amani ya Camp David yaliyotiwa saini kati ya Misri na utawala wa Kizayuni wa Israel. Hatua ya serikali ya Misri ya kukataa pendekezo hilo, hivi karibuni ilipelekea hata Washington kutuma ujumbe maalumu ulioongozwa na Seneta John Mc Cain kuwashawishi viongozi wa Cairo kufungamana na makubaliano ya Camp David. Baadhi ya viongozi wa Misri wamesikika wakisema kuwa, siyo jambo la kimantiki kwa Cairo kufungamana na makubaliano hayo.
Makubaliano ya amani ya Camp David yalitiwa saini kati ya Anwar Sadat Rais wa zamani wa Misri na Menachem Begin Waziri Mkuu wa zamani wa utawala wa Kizayuni wa Israel tarehe 17 Septemba 1978, chini ya usimamizi wa Jimmy Carter Rais wa zamani wa Marekani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO