Duru za kidiplomasia kutoka Cairo zinaeleza kuwa, serikali ya Misri 
imetupilia mbali takwa la Marekani la kuitaka serikali hiyo ifungamane 
kikamilifu na makubaliano ya amani ya Camp David yaliyotiwa saini kati ya Misri 
na utawala wa Kizayuni wa Israel. Hatua ya serikali ya Misri ya kukataa 
pendekezo hilo, hivi karibuni ilipelekea hata Washington kutuma ujumbe maalumu 
ulioongozwa na Seneta John Mc Cain kuwashawishi viongozi wa Cairo kufungamana na 
makubaliano ya Camp David. Baadhi ya viongozi wa Misri wamesikika wakisema kuwa, 
siyo jambo la kimantiki kwa Cairo kufungamana na makubaliano hayo.

No comments:
Post a Comment
TUPE MAWAZO YAKO