Saturday, January 26, 2013

WATANO WAUAWA MISRI KWENYE MAANDAMANO


Taarifa kutoka nchini Misri zinaeleza kuwa watu watano wameuawa na wengine kwa mamia wamejeruhiwa wakati wa maandamano ya kuadhimisha miaka miwili ya mapinduzi yaliyouondoa madarakani utawala wa Hosni Mubarak. Polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi dhidi ya waandamanaji waliokuwa nje ya makaazi ya rais mjini Cairo. Ghasia zilizosababisha vifo na majeruhi hao zimetokea mjini Cairo na Alexandria pamoja na miji mingine ya Misri. Rais Mohammed Morsi ametoa wito wa kuwepo utulivu baada ya ghasia kati ya wapinzani na askari polisi.
Maandamano hayo yaliyoitishwa na viongozi wa upinzani yanaipinga serikali ya Rais Morsi aliyechaguliwa kwa kuzingatia demokrasia na anayeungwa mkono na vyama vya itikadi kali za Kiislamu. Upinzani unamshutumu Rais Morsi kwa kusaliti mapinduzi hayo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO