Friday, January 25, 2013

WAPALESTINA KUISHITAKI ISRAEL ICC

Mamlaka ya Ndani ya Palestina imetishia kuichukulia Israel hatua za kisheria katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) iwapo Tel Aviv itajenga nyumba mpya katika maeneo ya Palestina inayoyakaliwa kwa mabavu. Riyad al Maliki Waziri wa Mambo ya Nje wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema hayo baada ya kushiriki kwenye mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York. Ameongeza kuwa, iwapo Israel itaendelea kujenga vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni pamoja na mipango mingineyo katika mji wa Baitul Muqaddas, Palestina itaifungulia mashtaka katika mahakama ya ICC kwani haitakuwa na chaguo jingine.
Utawala wa Kizayuni wa Israel unapanga kupanua vitongozi vya walowezi wa Kizayuni katika maeneo ya Palestina unayoyakalia kwa mabavu pambizoni mwa Quds Mashariki, suala ambalo ni kinyume cha maazimio na sheria za kimataifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO