Thursday, February 28, 2013

ALIYEMUUA KIONGOZI WA TUNISIA AJULIKANA

Waziri Mkuu mpya wa Tunisia, Ali Larayedh amesema kuwa, aliyemuua kiongozi wa upinzani Shokri Belaid majuma mawili yaliyopita amejulikana na kwamba vyombo vya usalama vinaendelea kumtafuta. Larayedh amesema uchunguzi umebaini kwamba Mawahabi wenye misimamo ya kufurutu ada ndio waliotekeleza mauaji hayo lakini akakanusha madai kwamba serikali ilihusika na mauaji hayo. Belaid ambaye alikuwa mkosoaji mkubwa wa serikali aliuawa kwa kupigwa risasi alipokuwa akitoka nyumbani kwake. Kuhusu suala la kuunda serikali mpya, Waziri Mkuu huyo amesema anaendelea kujadiliana na vyama pamoja na makundi mbalimbali ili serikali itakayoundwa iwe na sura ya kitaifa. Kiongozi huyo ambaye hapo awali alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wiki iliyopita kufuatia kujiuzulu mtangulizi wake, Hamad Jebali.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO