Thursday, February 28, 2013

MAREKANI KUONGEZA MISAADA KWA WASYRIA

Msemaji wa White House Jay Carney amesema kuwa, Marekani itaongeza misaada kwa waasi wanaopigana na serikali ya Syria eti kwa lengo la kuharakisha mabadiliko ya kisiasa katika nchi hiyo.
Matamshi hayo yametolewa huku gazeti la Washington Post likiandika kuwa, White House inaazimia kuwatumia waasi wa Syria silaha, magari ya kijeshi na ikiwezekana pia kuwapatia mafunzo ya kijeshi. Marekani imekuwa ikiwafadhili waasi wa Syria kwa lengo la kumuondoa madarakani Rais Bashar al Assad wa nchi hiyo.
Katika upande mwingine mwakilishi wa Syria katika Umoja wa Mataifa amewataka wanaojiita 'Marafiki wa Syria' kuwashauri wapinzani kukaa kwenye meza ya mazungumzo ya kitaifa na serikali bila masharti. Bashar al Jaafar amesema, iwapo kweli watu hao ni marafiki wa kweli wa taifa la Syria na wanajali wananchi wa nchi hiyo wanapaswa kuwashauri wapinzani kufanya mazungumzo ya kusitisha mapigano na kutoharibu zaidi miundombinu ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO