Saturday, February 23, 2013

ARAB LEAGUE YALAANI UKANDAMIZAJI UNAOFANYWA NA ISRAEL

Jumuiya ya Nchi za Kiarabu Arab League imelaani vikali siasa zisizo za kibinaadamu zinazofanywa na utawala haramu wa Kizayuni dhidi ya mateka wa Kipalestina. Akiashiria kuendelea kugoma kula mateka wa Kipalestina Samir al-Issawi anayeshikiliwa katika jela za kutisha za utawala huo, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) Muhammad Sabih amesema kuwa, viongozi wa Israel hawaitilii umuhimu wowote hali ya mateka huyo. Ameelezea hukumu ya hivi karibuni ya utawala katili wa Kizayuni, iliyosisitiza juu ya kucheleweshwa ufatiliaji wa kesi ya al-Isawi na kuitaja hukumu hiyo kuwa ya kifo dhidi ya mateka huyo wa Kipalestina ambaye alianza kugoma kula chakula tangu siku 215 zilizopita.
Al-Issawi alichukua uamuzi huo ili kulalamikia siasa za ukandamizaji zinazofanywa na utawala dhalimu wa Kizayuni. Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu pia amesisitizia udharura wa kufanyika juhudi za dhati zitakazosaidia kuachiliwa huru mateka wa Kipalestina hususan al-Isawi na kuongeza kuwa jumuiya hiyo itawasilisha kadhia hiyo kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binaadamu Human Right Watch na taasisi nyingine za kimataifa ili kuushinikiza utawala wa Kizayuni uheshimu haki za mateka hao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO