Saturday, February 23, 2013

MAREKANI NA NJAMA ZA KUIMALIZA HIZBULLAH

Mtandao wa habari wa al-Manar umeandika kuwa, Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel, zinafanya njama za kuimaliza Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon, Hizbullah. Al-Manar imeongeza kuwa, Marekani kwa kushirikiana na utawala wa Kizayuni na baadhi ya nchi za Kiarabu, zimeshadidisha njama zao za kuizingira harakati hiyo. Mtandao huo umeongeza kuwa, Marekani, Israel na baadhi ya nchi za Kiarabu katika eneo la Mashariki ya Kati zinafanya mawasiliano ya siri baina yao kwa ajili ya kuzuia uwezo wa Hizbullah kupitia mgogoro wa Syria. Pia umeandika, mawasiliano  hayo yanafanyika kwa kiwango cha hali ya juu na kwa siri, na  yanasimamiwa na Washington. Tangu utawala wa Kizayuni ulipopata kipigo kikali katika vita vya siku 33 kutoka kwa harakati hiyo ya Hizbulla, umekuwa ukifanya kila liwezekanalo kujaribu kuinyanganya Hizbullah silaha zake, suala ambalo limeshindikana kabisa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO