Saturday, February 23, 2013

MISRI YAKANUSHA JUU YA USHIRIKIANO WAKE NA ISRAEL

Msemaji wa Jeshi la Misri amekadhibisha habari za kuwepo mashirikiano ya kijeshi kati ya jeshi la nchi hiyo na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa lengo la kuharibu njia za chini kwa chini zilizoko katika mpaka kati ya Misri na Ukanda wa Ghaza. Ahmad Muhammad Ali amesisitiza kuwa, Misri haijafanya mazungumzo yoyote na utawala wa Israel kuhusiana na suala hilo. Amesema kuwa, jeshi la Misri lilianza kuharibu njia hizo za chini kwa chini baada ya watu wanaobeba silaha katika eneo la Rafah kuwauwa wanajeshi 16 wa Misri mwezi Agosti mwaka 2012. Msemaji wa Jeshi la Misri ameongeza kuwa, operesheni hiyo  bado inaendelea. Baada ya utawala wa Kizayuni wa Israel kuweka mzingiro dhidi ya wananchi wa Ukanda wa Ghaza tokea mwaka 2006, wananchi wa Gaza walitengeneza  mamia ya njia za chini kwa chini kwa lengo la kupitisha mahitajio yao muhimu kama vile madawa, chakula na vifaa vya ujenzi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO