Saturday, February 23, 2013

ASKARI WA ISRAEL WAWAJERUHI WAPALESTINA


Askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewalenga risasi na kuwajeruhi Wapalestina 35 waliokuwa wakiandamana katika mji wa al Khalil kwenye Ukingo wa Magharibi mwa Mto Jordan. Wapalestina hao walikuwa wakiandamana baada ya Sala ya Ijumaa ya leo ili kuonyesha mshikamano wao kwa mateka wa Palestina wanaogoma kula katika jela za Israel. Askari wa Israel katika kuzuia maandamano hayo ya amani ya Wapalestina waliwashambulia na kuwajeruhi 35 miongoni mwao.
Katika upande mwingine wanajeshi wa Israel tangu leo asubuhi walimiminika katika mji wa Quds na kuwashambulia Wapalestina waliokwenda kuswali kwenye msikiti wa al Aqswa kwa gesi za kutoa machozi.  Hayo yamejiri sambamba na kushuhudiwa maandamano katika maeneo tofauti ya Palestina ya kuunga mkono mateka wa Kipalestina wanaoshikiliwa  bila kujulikana makosa yao katika jela za kuogofya za Israel.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO