Saturday, February 23, 2013

TUNISIA YAPATA WAZIRI MKUU MPYA


Rais Moncif Marzouki wa Tunisia amekubali uteuzi wa Ali Larayedh aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo kama Waziri Mkuu mpya atakayechukua nafasi ya Hamadi Jebali aliyejiuzulu. Larayedh ni miongoni mwa waasisi wa chama cha an Nahdha na amependekezwa na chama hicho kushika wadhifa huo.  Hivi sasa Larayedh atakuwa na siku 15 za kuunda serikali mpya na kuwasilisha mpango wake wa kuongoza serikali. Pia Rais Marzouki amemtaka Waziri Mkuu huyo mpya wa Tunisia kuunda serikali haraka iwezekanavyo akisisitiza kwamba nchi hiyo haiwezi kusubiri tena suala hilo.
Hamadi Jebali alitangaza kujiuzulu Jumanne baada ya mpango wake wa kuunda serikali inayowajumusiha wataalamu mbalimbali kufeli, mpango ambao ulianza kupingwa ndani ya chama chake cha an Nahdha. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO