Saturday, February 23, 2013

IRAN YALAANI MRIPUKO WA DAMASCUS


Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali shambulio la kigaidi lililolenga makaazi ya raia na kusababisha watu 53 kuuawa na wengine 250 kujeruhiwa katika mji mkuu wa Syria, Damascus. Taarifa ya wizara hiyo imesema kuwa, wanaolitakia mema taifa la Syria wanatiwa wasiwasi na kuendelea kukosekana amani na usalama nchini humo na kutoa wito wa kufanyika mazungumzo ya kitaifa badala ya kutumiwa mtutu wa bunduki. Taarifa hiyo pia imesisitiza kwamba vitendo kama hivyo vinaendelea kutekelezwa na magaidi wanaofadhiliwa na madola ya kigeni kwa lengo la kukwamisha jitihada za kutekeleza mageuzi ya kisiasa na kurejesha amani na usalama nchini Syria.
Wakati huo huo Russia imekosoa msimamo wa kindumilakuwili wa Marekani kuhusiana na Syria na kuilaumu Washington kwa kuzuia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kulaani mlipuko huo wa bomu uliotokea mjini Damascus.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO