Thursday, February 21, 2013

HAGUE UKO ZIAANI LEBAON

Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague yuko Lebanon kujadili juu ya mzozo unaoendelea nchini Syria pamoja na suala la kuimarisha mahusiano baina ya Uingereza na Lebanon. Hague alikutana na rais wa Lebanon Michel Suleiman na atakutana pia na Mkuu wa majeshi wa nchi hiyo Jenerali Jean Kahwagi. Hague aliyewasili Lebanon Jumatano jioni akitokea Qatar, aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa atajadili katika mazungumzo yake na maafisa wa Lebanon kuhusu hali ya kisiasa nchini humo pamoja na mzozo wa syria. Ziara ya kiongozi huyo inafanyika wakati huu kukiwa na hali ya wasiwasi katika mpaka wa Lebanon na Syria unayowahusisha waasi wa Syria pamoja na kundi la Hezbollah la Lebanon ambalo ni mshirika mkubwa wa utawala wa rais Bashar al-Assad.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO