Thursday, February 21, 2013

UJERUMANI YAWASHITAKI WALIOIPA IRAN NDEGE ZAKE


Raia wawili wa Iran wamefunguliwa mashitaka kwa tuhuma za kusafirisha kwa njia haramu ndege za kivita zilizotengenezwa Ujerumani kwa ajili ya kutumiwa katika uchunguzi wa ndege ya kivita ijulikanayo kama Ababil 3 pamoja na ndege zisizokuwa na rubani. Ujerumani inakataza usafirishaji wa zana zake za kijeshi nchini Iran ambazo zinaweza kutumiwa kijeshi kinyume na hivyo kwenda kinyume na vikwazo vya kimataifa vilivyowekwa dhidi ya taifa hilo. Watu hao ambao mmoja ana uraia wa Iran na Ujerumani na mwingine mwenye uraia wa Iran wamefunguliwa mashitaka ya kukiuka sheria za usafirishaji za Ujerumani. Ababil 3 inaaminika kuwa na ukubwa wa kilometa 145 na inaweza kuruka angani katika umbali unaofikia mita 4,300. Ndege hiyo imetengenezwa kwa ajili ya uchunguzi na masuala ya ukusanyaji taarifa za kijasusi, ingawa waendesha mashitaka nchini Ujerumani wanasema kuwa inawezekana pia zikatumika kama ndege za mashambulizi zisizokuwa na rubani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO