Thursday, February 21, 2013

WAASI WA SYRIA WATISHIA KUISHAMBULIA HIZBOLLAH

Kamanda wa jeshi huru la waasi wa Syria, FSA, Jenerali Selim Idriss, ametoa muda wa masaa 48 kwa kundi la Hezbollah la Lebanon kuacha kuzishambulia ngome zinazoshikiliwa na waasi la sivyo watalishambulia kundi hilo. Kitisho hicho kimetolewa jana baada ya waasi kuishambulia ndege ya kivita ya serikali kufuatia shambulizi kubwa lililouwa watu 20 mjini Damasucus. Jenerali Idriss ameliambia shirika la habari la AFP kuwa kundi la Hezbollah limekuwa likijihusisha kwa muda mrefu na mapigano yanayoendelea nchini Syria, lakini sasa limevuka mipaka kwa kuvishambulia vijiji vilivyo karibu na eneo la Qusayr kwenye mji wa Homs. Kundi la Hezbollah limekanusha kuhusika na mashambulizi hayo ingawa mwezi Oktoba mwaka uliopita kiongozi wake Hassan Nasrallah alikiri kuwa baadhi ya wanamgambo wake waliwashambulia waasi wa syria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO