Thursday, February 21, 2013

HAMAS YAITAKA ISRAEL IFUATE UTARATATIBU WA KUBADILISHANA MATEKA

Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeuonya utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusiana na kukiuka mkataba wa ubadilishanaji mateka. Sami Abu Zuhri, msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS ameitahadharisha Israel na kusisitiza kwamba, utawala huo ghasibu unapaswa kutazama upya, tena haraka iwezekanavyo uamuzi wake wa kutaka kuwatia mbaroni tena mateka wa Kipalestina walioachiliwa huru. Sami Abu Zuhri amesema, Hamas inautaka utawala huo ufikirie upya uamuzi wake huo kabla haujajuta. Wakati huo huo, Sami Abu Zuhri, Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amezikosoa vikali siasa za kindumakuwili za Marekani kuhusiana na kadhia ya Palestina na kusisitiza kwamba, Washington inakwamisha mwenendo wa utekelezwaji makubaliano ya maridhiano ya kitaifa huko Palestina.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO