Thursday, February 21, 2013

WAZIRI MKUU WA TUNISIA AJIUZULU

Hamad Jebali Waziri Mkuu wa Tunisia jana alitangaza kujiuzulu kufuatia mgogoro wa kisiasa unaoikabili nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika. Jebali alitangaza kuchukua hatua hiyo baada ya kushindwa katika jitihada zake za kuunda serikali mpya ya kiteknokrasia yaani inayowajumuisha wataalamu wa taaluma mbalimbali badala ya wanasiasa. Jebali alisema baada ya kukutana na Rais Munsif Marzouq kama ninavyomnukuu:"niliahidi na kutoa hakikisho kuwa nitajiuzulu wadhifa huu nilionao wa mkuu wa serikali iwapo juhudi zangu zitashindwa, na ndivyo nilivyofanya",mwisho wa kunukuu. Jebali  hata hivyo amesema kuwa kushindwa kwa juhudi zake hakumaanishi kushindwa Tunisia au kushindwa mapinduzi ya Januari mwaka 2011 yaliyomuondoa madarakani dikteta wa nchi hiyo Zainul Abidin bin Ali. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO