Thursday, February 21, 2013

WAMAGHARIBI HAWALIONI SUALA LA MYANMAR


Mjumbe wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Nje wa Bunge la Iran ameashiria ripoti ya Umoja wa Mataifa juu ya kukiukwa haki za Waislamu wa Myanmar na kusema kuwa, siasa za kindumilakuwili za Wamagharibi kuhusu haki za binadamu na kulinda utu wa mwanadamu zimechangia katika mauaji ya Waislamu wa Myanmar.
Hussein Subhani-niya ameongeza kuwa wakati magaidi wanaoungwa mkono na nchi za Magharibi wanapotenda jinai huko Syria, Iraq, Pakistan na Afghanistan nchi hizo pia hunyamaza kimya, suala linaloonesha kwamba Wamagharibi ndio waungaji mkono wakuu wa magaidi duniani. Amesema, kuuawa bila hatia Waislamu wa Myanmar ni mfano wa wazi wa kukiukwa haki za walio wachache katika nchi hiyo.
Wakati huo huo Tomas Ojea Quintana, mwakilishi maalum wa UN katika masuala ya haki za binadamu pia mwishoni mwa safari yake ya siku 5 huko Myanmar amesema kwamba, licha ya madai ya serikali ya kufanya mabadiliko nchini humo lakini bado Waislamu wanadhulumiwa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO