Saturday, February 23, 2013

SPIKA WA BUNGE LA LEBANOPN AIONYA VIKALI ISRAEL

Spika wa Bunge la Lebanon Nabih Berri, ameuonya vikali utawala wa Kizayuni wa Israel kutokana na kupora utajiri wa mali ya Lebanon. Nabih Berri amesema kuwa, utawala ghasibu wa Kizayuni unafanya njama za kupora utajiri wa nchi hiyo kwa kutumia vibaya tofauti zilizopo kati ya ulimwengu wa Kiarabuhivi sasa. Ameukumbusha utawala huo kuwa, haupaswi kusahau kwamba, ipo Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya nchi hiyo, ambayo itasimama kidete kutetea haki na mali za Lebanon. Onyo hilo linatolewa wakati ambapo kwa mara kadhaa viongozi wa serikali ya Beirut walikwishaionya vikali Israel kuhusiana na kuendelea kupora utajiri wa mafuta na gesi vya nchi hiyo. Mbali na hayo, viongozi wa Beirut wametaka Umoja wa Mataifa kuushinikiza utawala huo wa Kizayuni ili ukomeshe mara moja kupora utajiri wa Lebanon.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO