Sunday, February 24, 2013

WAFUNGWA WA KIPALESTINA WAGOMEA CHAKULA ISRAEL


Wapalastina kadiri 3000 wanaoshikiliwa katika jela za Israel wameanzisha mgomo wa siku moja kususia chakula hii leo waakilalamika dhidi ya kufariki dunia mwenzao aliyekuwa korokoroni-kisa hicho kimezusha mapigano kati ya vikosi vya usalama  vya Israel na waandamanaji katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.Msemaji wa shughuli za jela za Israel Sivan Weizman ameliambia shirika la habari la Ufaransa AFP  tunanukuu" ni chakula cha siku moja tu-"Arafat Jaradat,aliyekuwa na umri wa miaka 30 amekufa kwa ghafla jana akiwa jela,katika kile ambacho maafisa wa jela wanasema pengine kimesababishwa na kusita mipigo ya moyo.
Waandamanaji katika mji wa kusini mwa Ukingo wa magharibi-Hebron wanawavurumishia mawe wanajeshi wa Israel wanaoajibu kwa kufyetua gesi za kutoa machozi na kuvurumisha maguruneti.Hakuna  bado ripoti kuhusu majeruhi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO